Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Friday, October 17, 2014

NEWCASTLE KUPIMA WACHEZAJI WAO WAAFRIKA KUTOKANA NA EBOLA




ALAN-PARDEW-MASHANI
Kocha wa Newcastle united Alan Pardew
NEWCASTLE imeamua kuchukua hatua kujikinga na Ugonjwa wa Ebola kwa kuwapima Wachezaji wao wanaorejea Klabuni baada ya Mechi za Kimataifa toka Barani Afrika.

Gonjwa la Ebola limeikumba Afrika Magharibi na kuua Watu zaidi ya 4,000 na hivi sawa huko Uingereza Vituo vya Forodha vya Majini na kwenye Ndege Watu hupimwa Ugonjwa huo.
Sasa Klabu ya Newcastle nayo imeamua kuwapima Wachezaji wao Waafrika wanaorejea Klabuni baada ya kucheza Mechi za Kimataifa na Nchi zao.

Wachezaji wa Newcastle, Papiss Cisse, anaetoka Senegal, na Cheik Tiote, wa Ivory Coast, walikwenda Nchini mwao na pia kusafiri na Timu zao kucheza Mechi za Makundi za AFCON 2015 huko Tunisia na Congo DR.
Meneja wa Newcastle, Alan Pardew, amekiri Klabu yao watakuwa wapuuzi ikiwa hawaukubali Ugonjwa huo.

: “Tunao mkakati wakirudi wao na Familia zao wataangaliwa. Hii ni kuwalinda na kuwasaidia.”alisema Pardew.

Lakini pia nchi 3 tayari zilishapigwa marufuku na CAF kucheza Mechi kwao baada ya kuvamiwa na Ugonjwa huu na hizo ni Liberia, Guinea na Sierra Leone.

_________LIGI KUU ENGLAND

RATIBA-Mechi zijazo:
**Saa za Bongo

Jumamosi Oktoba 18
 1445 Man City v Tottenham

1700 Arsenal v Hull

1700 Burnley v West Ham

1700 Crystal Palace v Chelsea

1700 Everton v Aston Villa

1700 Newcastle v Leicester

1700 Southampton v Sunderland

Jumapili Oktoba 19

1530 QPR v Liverpool

1800 Stoke v Swansea

Jumatatu Oktoba 20

2200 West Brom v Man United





0 comments: