Picha za ngono zilizozagaa katika mitandao ya kijamii za Staa wa Bongo
Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, zikimuonesha akifanya ufuska
na mrembo chumbani zimemliza mchumba’ke, Siwema ambaye ameamua kumsusia
mtoto wao mchanga.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika zilimiminika kwamba, baada ya
kusambaa kwa picha hizo kuliibuka tafrani nyumbani kwa wapenzi hao,
Kimara jijini Dar ambapo Siwema alidai kuondoka usiku wa manane
akimwacha mtoto mchanga.
Nay ALITAFUTWA ili kuzungumzia
sakata hilo ambapo alikiri kuzijua picha hizo lakini akashangaa ni nani
aliyempenyezea umbeya mchumba’ke na kwamba ni kweli mama mtoto wake huyo
alilia japokuwa alitumia nguvu kubwa kumweka sawa na sasa maisha
yanaendelea.
Kwa upande wa Siwema alisema: “Nay amenipa maelezo juu ya picha hizo
ingawa tulikuwa tumefikia pabaya sana kiasi cha kutaka kuondoka kwake
lakini kanielewesha.
0 comments:
Post a Comment