LICHA ya tetesi za kila siku kuhusu uwezekano wa kusajili wachezaji nyota, Manchester United imeshindwa kufanya usajili wowote katika siku ya mwisho ya dirisha dogo la Januari.
Manchester United imeishia kuuza wachezaji wake kadhaa huku ikiwatoa wengine kwa mkopo lakini ni kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdes na beki kinda Sadiq El Fitouri ndiyo wanakuwa wachezaji pekee waliosajiliwa Old Trafford katika kipindi hiki ambacho United ilihitaji sana kuimarisha safu yake ya ulinzi.
Katika hali inayoshangaza, Manchester United imemsajili kwa mkopo beki Andy Kellett kutoka Bolton Wanderers.
Hata hivyo beki huyo mwenye umri wa miaka 21 aliyefanikiwa kuichezea Bolton mechi moja tu, atakitumikia kikosi cha United chini ya miaka 21 hadi mwezi Juni.
Baada ya kumtumia kwa jumla dakika 26 tu kwenye mechi za Premier League, United imemuuza jumla Wilfried Zaha kwa timu yake ya zamani Crystal Palace.
Kiungo Darren Fletcher nae pia ameondoka Old Trafford katika siku ya mwisho ya dirisha la usajili na kujiunga na West Bromwich Albion wakati Anderson anarejea kwao Brazil.
Kiungo chipukizi wa United Saidy Janko amepelekwa Bolton Wanderers kwa mkopo huku kiungo mwingine Jesse Lingard naye akijiunga na Derby County kwa mkopo wa hadi mwisho wa msimu.
0 comments:
Post a Comment