Waziri wa usalama nchini Kenya Joseph Nkaissery amewaomba radhi wanafunzi wa shule ya msingi waliofyatuliwa gesi ya kutoa machozi wakati walipokuwa wakiandamana kupinga unyakuzi wa kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.
Nkaisery ameongeza kwamba serikali itaweka uzio katika ardhi hio na kuiwacha kuwa uwanja wa kuchezea wa wanafunzi hao.
Wakenya wamekosoa polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya wanafunzi , hali ambayo imesababisha afisa ammoja mkuu kusimamishwa kazi kwa mda.
Shirika la kutetea masilahi ya watoto, la Save The Children, pia limelaani kitendo cha polisi dhidi ya wanafunzi hao ambao walikuwa wanaandamana kwa amani kutetea uwanja wao uliokuwa umenyakuliwa.
0 comments:
Post a Comment