Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Sunday, October 26, 2014

TAMASHA LA SIKU YA MSANII MLIMANI CITY MATAWI YA JUU HAIJAWAHI KUTOKEA! …pata picha za matukio mbali mbali




TAMASHA la Siku ya Msanii lililofanyika jijini Dar es Salaam jana usiku, litaendelea kubakia kwenye historia ya aina yake baada ya kubeba hadhii ya kipekee – lilikuwa ni tamasha bab kubwa, mandhar bab kubwa, show bab kubwa, mgeni rasmi bab kubwa, tuzo bab kubwa.
Mgeni rasmi katika tamsha hilo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt  Mohammed Gharib Bilal.
Aina ya watu waliojazana ukumbuni, aina ya mavazi yalitotawala ukumbini, aina ya burudani zilizotolewa na nidhamu iliyokuwepo, inafanya tamasha hilo lililofanyika Mlimani City, liwe sahihi kwa watu wa rika zote – wakubwa na wadogo.
Zikatolewa tuzo mbili mahsusi: Tuzo ya msanii aliyejitolea maisha yake yote katika sanaa ambayo ilikwenda kwa mchoroji maarufu Edward Said Tingatinga mwenye maskani yake Masasi mkoani Mtwara. Tuzo ya pili ni ya msanii aliyetumia sanaa kuitumikia jamii kwa maisha yake yote ambayo ilikwenda kwa Father Kanuti, mmoja wa watu waliowafundisha wanamuziki wengi sana hapa nchini.
Siku ya msanii Siku Ya Msanii iliandaliwa na Haak Neel Production kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kudhaminiwa na New Habari |(2006) LTD kupitia magazeti ya Dimba, Bingwa, Mtanzania na The African, Azam Media, Ledger Plaza Hotel, CXC, Proin Tanzania, Channel Ten, Magic FM, Clouds FM, EFM.
Washindi wa tuzo walipewa bakshishi ya shilingi milioni moja kila moja, lakini kama vile hiyo haitoshi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt  Mohammed Gharib Bilal akawaongeza milioni tano kila moja na kufanya kila mshindi aende nyumbani na kitita cha shilingi milioni 6.
Burudani zilizorindima ukumbini mbali na sarakasi na ngoma za asili na show za madansa, pia kulikuwa na uhondo kutoka kundi la The Kilamanjaro Band “Wana Njenje”, Isha Mashauzi, Diamond, Yamoto Band na wavunja mbavu kutoka Kenya Erick Omondi na Fred Omondi.
Lakini tamasha hili ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka Oktoba 25, lilipambwa pia na maonyesho ya mavazi yaliyoandaliwa na Fabak Fashion chini yake Asiya Idarus.
Pata picha kadhaa za tamasha hilo la aina yake.
 Safu ya viongozi wa serikali ikifuatilia tamasha la Siku ya Msanii
 Madansa wa Extra Bongo chini ya Super Nyamwela
 Hiyo ni tuzo aliyopewa Father Kanuti
 Isha Mashauzi akipiga bonge la show

 Mashauzi na madansa wake wakiendelea na makamuzi
 Ni wakati wa fashion show
Ako Mpiluka Band wakali wa kupiga nyimbo za asili kwa kutumia ala za kisasa
 Mwanaume kazini!
 Uhondo wa ngoma za utamaduni


MC wa tamasha la Siku ya Msanii Jokate (kushoto) akinyongesha kiuno na Nyota Waziri

 Nyota Waziri akifanya yake
Ni wakati wa Diamond kufanya yake

 Diamond akiendelea kupagawisha
Kazi bado inaendelea kwa Diamond na mashabiki wake
 Si mchezo
Si uchawi ni mazoezi
Tingatinga akipokea tuzo yake kutoka kwa Makamu wa Rais
Wachekeshaji kutoka Kenya
 Achana kabisa na hawa watu
 Yamoto Band wakishambulia jukwaa
Yamoto Band
 Si chura huyu, ni binadamu
 Jamaa alijua kucheza na mwili wake
Fashion haina umri wala umbo! hapo ni mwanamuziki Abdul Salvador,Asia Idaurus

Related Posts:

0 comments: