Msanii wa muziki, Bob Junior akifanya yake jukwaani. Mdada akipagawa na wimbo wa msanii Shebby Love (kushoto). Msanii Ben D akiwa na wacheza shoo wake. Mashabiki wakijiachia kwa burudani. Wacheza shoo wa Club 71 wakitoa burudani.…Akiwa kwenye pozi na mashabiki. Msanii Mabeste (mwenye shati ya njano) akiwa na baadhi ya uongozi wa Club 71 ya Tegeta jijini Dar.
WASANII kibao jana
walijitokeza kumuunga mkono msanii Mabeste katika shoo maalum kwa ajili
ya kuchangia fedha za matibabu ya mkewe, Lisa Karl ambaye pia ni meneja
wake.
Shoo hiyo iliyopewa jina la ‘Mrs Mabeste
Charity Show Club 71’ ilifanyika usiku wa jana katika club hiyo iliyopo
Tegeta, jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wasanii waliohudhuria ni pamoja
na Bob Junior, Top In Dar ‘TID’, Ben D, Shebby Love, Sting Wera Wera
toka Kenya na wengineo.
0 comments:
Post a Comment