Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Monday, November 10, 2014

NOMA:HII ndio mijengo kumi ya mastaa wa SOKA hapa duniani__NI NOMAA


Kuna mijengo kibao ya thamani ya wanasoka, lakini hapa tunakuletea mijengo 10 iliyo na thamani zaidi, hebu itupie macho a moja baada ya jingine.
1. David Beckham: $20 million
David Beckham anamiliki mijengo kibao ya gharama, mmoja kati ya hiyo ni ule alioupa jina la “Beckingham Palace” uliopo katika Jiji la London ukiripotiwa kuwa na thamani ya dola milioni 20. Aliununua mwaka 1999. Pamoja na mambo mengine, una chumba cha kufanyia ibada, studio ya kurekodia muziki na uwanja wa soka.
2. Wayne Rooney: $17.83 million
Wayne Rooney anayeishi katika eneo la Cheshire katika Jiji la Manchester akiwa jirani na nyota wenzake kama Robin van Persie na Rio Ferdinand, mjengo wake una thamani ya karibu dola milioni 17.83 – kiwanja peke yake kina thamani ya dola milioni 1.57. Mjengo huo uliojengwa mwaka 2004, una bwawa kubwa la kuogelea, ukumbi binafsi wa burudani, eneo la sanamu za utamaduni wa kigiriki, na mfumo maalumu wa kutengeneza joto ardhini wakati wa barini katika bustani. Wazza pia amefunga kamera zenye mfumo wa kurekodi kwa siri matukio mbalimbali (CCTV) kwa thamani ya karibu dola 48,800.
3. Didier Drogba: $9 million
Didier Drogba mwenye utajiri wa dola milioni 20.8 kwa mujibu wa Forbes, anamiliki mjengo wenye thamani ya dola milioni 9 uliojengwa mwaka 2007 ukiwa kwenye eneo la mita za mraba 799. Una bafu nane, vyumba vya saba vya kulala na chumba cha kuwekea mataji.
4. John Terry: $7.5 million
Kwa sasa, John Terry bado ni mchezaji maarufu wa Chelsea licha ya kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Uingereza. Anamiliki mjengo wenye thamani ya dola milioni 7.5, ambao ulikuwa sokoni huko nyuma. Una ukumbi binafsi wa sinema wenye uwezo wa kuchukua watu 34 na vyumba 10 vya kulala.
5. Frank Lampard: $7 million
Nyota wa zamani wa Chelsea anayecheza kwa mkopo Manchester City, Frank Lampard anamiliki mjengo wenye thamani ya dola milioni 7 ukiwa kwenye eneo la mita za mraba 1,812. Mjengo huu una vyumba tisa vya kulala, bafu 12, uwanja wa gofu, bwawa la kuogelea, uwanja wa tenisi na hata kizimba cha boti.
6. Cristiano Ronaldo: $6 million
Mjengo wa Cristiano Ronaldo ulio katika Jiji la Madrid aliununua mwaka 2008 kwa bei ya dola milioni 6. Una gym, pool, sauna, gym, bwawa la kuogea, sehemu maalumu ya kuhifadhia samaki kwa ajili ya kujiburudisha kwa kuwatazama na ukumbi binafsi wa burudani.
7. Mario Balotelli: $4.86 million
Kwa sasa Mario Balotelli haishi katika mjengo huu wenye thamani ya dola milioni 4.86. Ameupangisha kwa pango ya dola 21,930 kwa mwezi baada ya kuondoka Manchester City kwenda AC Milan mwaka jana. Mjengo huu una bwawa la kuogelea, baa, ukumbi binafsi wa burudani, uwanja wa kuchezea gofu, vyumba vinne vya kulala na vya kuogea.
8. Andres Iniesta: $4.6 million
Staa huyu wa Barcelona na Hispania anamiliki mjengo wenye thamani ya dola milioni 4.6. Mjengo huu unaonekana mdogo kwa nje, lakini kwa ndani ni tofauti: una vyumba vitano vya kulala, bwawa la kuogelea na chumba cha kufanyia ibada ikizingatiwa kuwa ni muumini wa Kanisa Katoliki.
9. Kaka: $3 million
Ricardo Izecson dos Santos Leite – maarufu kwa jina la Kaka – ana mjengo ulio katika mita za eneo 139.4 jijini Madrid ukiwa na thamani ya dola milioni 3. Aliununua mwaka 2009 baada ya kujiunga na Real Madrid akitokea AC Milan. Pamoja na mambo mengine, una gym, bwawa la ndani la kuogelea, gereji yenye uwezo wa kuhudumia magari sita kwa wakati mmoja. Kwa sasa ameupangisha kwa supastaa wa Real Madrid, Gareth Bale kwa pango ya dola 16,000 kwa mwezi.
10. Lionel Messi: Thamani haijulikani
Mjengo wa Lionel Messi thamani yake haijawekwa wazi, lakini unastahili kumilikiwa na watu wa hadhi yake. Una spa, ukumbi binafsi wa burudani, uwanja wa ndani wa soka. Kwa sasa staa huyo ana mpango wa kujenga mjengo mpya wa kifahari ambao ramani yake ni kama uwanja wa soka unavyoonekana kutokea juu (tazama picha hapo chini).

0 comments: