Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Friday, October 31, 2014

WANANCHI WATAKIWA KUJISAJIRI KATIKA VIKUNDI ILI KUKOPESHWA MBOLEA




Kilimo ni uti wa mgongo kutokana na kwamba watanzania waliowengi ni wakulima lakini tatizo kubwa ambalo limekuwa likiwakabili wakulima hawa ni uhaba wa mbolea na pembejeo

Hata hivyo mbolea ambazo zimekuwa zikitolewa kwa njia ya ruzuku zimekuwa zikitafunwa na baadhi ya watendaji ambao siyo waminifu, pia wakibainika na ubadhirifu huo huhamishwa kutoka ofisi moja hadi nyingine.

Afisa wa takukuru mkoani iringa bw. Ismail Bukuku alisema viongozi wenye tabia ya kutafuna mali za serikali wakamatwe kama wala rushwa na siyo kuhamishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Na mbolea ambayo imekuwa ikitumiwa na wakulima ni mbolea ya minjingu ambayo hulalamikiwa na wakulima walio wengi kuwa haina ubora.

Wadau wa kilimo wameshauriwa kutoa elimu mara kwa mara kuhusu matumizi bora ya mbolea ya minjingu ili wakulima wafanye kazi kwa utaramu na siyo kubahatisha “Ameria galinoma diwani wa kata ya kalenga alisema,” kwa upande wake afisa kilimo wilaya ya Iringa Lucy nyalu alisema, elimu kuhusu matumizi ya mbolea ya minjingu imekuwa ikitolewa kupitia mashamba darasa.



Ni mkuu wa wilaya ya iringa Dr letisia warioba akiongea na madiwani pamoja na viongozi mengine katika ukumbi wa siasa ni kilimo uliopo halmashauri ya wilaya ya Iringa vijijini kuhusu kujisajiri katika vikundi ili wakopeshwe mbolea.


 Hata hivyo mwenyekiti wa kamati ya pembe jeo ambae pia ni mkuu wa wilaya ya Iringa Dr. letisia warioba alisema vikundi vitakavyo kopeshwa mbolea ni vile vilivyo sajiliwa tu, pia amewataka madiani wawahamasishe wananchi kujisajiri katika vikundi mbalimbali.

Aidha warioba aliahidi kutoa milioni moja (1) kwa wilaya ya iringa ili isaidie ujenzi wa maabara.

Related Posts:

0 comments: