Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Sunday, October 26, 2014

MARIO BALOTELLI AANZA KUMKATISHA TAMAA BRENDAN RODGERS, LIVERPOOL SASA YAJIPANGA KUMNASA SAIDO BERAHINO


Berahino in action for Baggies in the Capital One Cup against Oxford United
LICHA ya kuwa kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amekuwa akimkingia kifua mshambuliaji wake Mario Balotelli, lakini ni wazi kuwa kocha huyo sasa anaanza kuangalia mipango mingine ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji.
Baada ya Balotelli kukosa bao la wazi akiwa hatua tatu tu kutoka langoni katika mchezo wa Ligi Kuu wa sare ya 0-0 dhidi ya Hull City, ikiwa ni mechi ya pili mfululizo kupoteza nafasi ya wazi, Brendan Rodgers sasa anataka kumsajili Saido Berahino wa West Bromwich Albion.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa ‘Under 21’ ya England, amekuwa pia akiwaniwa na Tottenham Hotspur ambapo ofa ya pauni milioni 15 imekuwa ikihusishwa na klabu hiyo kutoka kaskazini mwa London.
Hata hivyo West Bromwich inaamini Berahino ana thamani ya pauni milioni 25 na ujio wa Liverpool kwenye mpango huo, utapelekea vita vya kuonyeshana nguvu ya pesa kati yao na Spurs.
Liverpool imebaini wazi kuwa kumsajili Balotelli ilikuwa ni kamari ambayo haijalipa na itaangalia uwezekano wa kummuvuzisha kwenye dirisha dogo la Januari.
Habari za ndani zinasema hata kama Liverpool watashindwa kumhamisha, lakini bado watasajili mshambuliaji mwingine.

Related Posts:

0 comments: