Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Tuesday, October 28, 2014

IRINGA : MFUKO WA PESHENI WACHANGIA BATI MIA MBILI WILAYA YA KILOLO



Mfuko wa pesheni wa PSPF umetoa msaada wa bati mia mbili (200) zenye thamani y ash. Milioni sita (6) za kitanzania kwa mkuu wa wilaya ya kilolo Bw. Gerrad Gurninita ambazo zitasaidia ujenzi wa maabara.

Makabidhiano hayo ya bati yalifanyika hapo jana mbele ya viongozi wa PSPF na waandishi wa habari katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya kilolo.
Gerard Guninita

Aidha mkuu wa wilaya ya Kilolo gerrad gurninita alisema msaada huo utasaidia kukamirisha ujenzi wa maabara katika shule zote za sekondari ambapo wanatarajia kukamirisha ujenzi huo ifikapo 30 novemba 2014

Guninita aliongeza kuwa miongoni mwa shule zitakazonufaika na msaada huo ni shule ya sekondari ya kiheka, iketa pamoja na shule ya sekondari ya lulanzi.

Pia alisema shule ambazo zimeshakamirisha ujenzi wa maabara ni shule ya sekondari ya madege iliyopo kata ya idete, masisiwe, mawambala, na shule ya sekondari ya kilolo lakini kwa upande wa shule ya lulanzi wameanza kujenga msingi.

Hata hivyo guninita aliwataka wananchi kuunga mkono katika ujenzi huo wa maabara kwa kutoa chochote walichonacho.

0 comments: