Hawa ni kati ya vijana wanaocheza michezo ya video. |
Imebainika kuwa mtu huyo aliaga dunia masaa kadhaa huku wenzake wakiendelea kucheza bila kujua.
Alipatikana amelala katika meza moja ndani ya mgahawa wa mitandao mnamo Januari 8 akiwa hana uhai na kulazimika kupelekwa hospitalini ambapo alitangazwa kwamba amefariki.
Vijana wanaocheza michezo ya mitandaoni |
Mtu huyo ambaye hakuwa na ajira alipendelea sana kutembelea migahawa ya mitandao polisi walisema.Inadaiwa kwamba mtu huyo angetoweka kwa siku mbili ama hata tatu kwa mara moja.
Maafisa wa Polisi wamesema kwamba wachezaji wa mchezo wa mtandao katika mgahawa huo waliendelea kucheza bila kugundua ni nini haswa kilichotokea licha ya maafisa hao pamoja na madktari kuwasili ili kumchunguza mtu huyo.
0 comments:
Post a Comment