Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Tuesday, January 20, 2015

GUINEA Pamoja na IVORY COAST _ kuwakosa Manahodha wao

kikosi cha timu ya Taifa Guinea
 Beki huyo wa kulia mwenye miaka 29 anayechezea klabu ya Sheffield Wednesday hakuweza kufanya mazoezi na wenzake kutokana na tatizo hilo la mguu.

Pia nahodha wa Ivory Coast Yaya Toure ambaye hakufanya mazoezi lakini kocha wake Herve Renard anasema baada ya hatua za tahadhari kuchukuliwa kiungo huyo yuko vizuri.

"Ameichezea Manchester City mechi nyingi haswa kati ya Krismasi na mwaka mpya, ila jambo muhimu ni jumanne,"alieleza Renard

Ivory Coast imepoteza nafasi zao mara kadhaa kama timu ilio juu Afrika wakiwa nafasi ya tatu nyuma ya Algeria na Tunisia.



kikosi cha timu ya Ivory Coast

 Lakini bado wanajivunia kuwa na kikosi bora chenye nguvu barani Afrika.
Kuwepo kwa ndugu Yaya Toure, kaka yake Kolo, Serge Aurier, Gervinho, Seydou Doumbia na Wilfried

Bony kunamfanya kocha Renard kuamini kuwa nyota hawa wa Tembo wa Afrika wanaweza kuukaribia ubingwa.

Mwaka 2012, Renard aliongoza Zambia kutwaa ubingwa,Sasa anataka kukiongoza kikosi chake kutwaa ubigwa.

0 comments: