Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Wednesday, November 12, 2014

IRINGA: WANANCHI MKOANI WATAKIWA KUWA MAKINI NA MAJANGA YA MOTO











 

Anaye onekana kwa mbele akitoa  maelezo ni Kennedy   komba kamanda wa kikosi cha zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa.               
 
Kamanda wa kikosi cha zima moto na uokoaji mkoani Iringa bw. bwana Kennedy Komba amewataka wananchi kuwa makini na moto unapotokea ili kuepuka madhara mengine ambayo yanaweza kujitokeza.

Wito huo ulitolewa kwa wananchi hapo jana katika kata ya makorongoni jirani na makorongoni geragi baada ya kikosi cha zima moto kuuzima moto uliokuwa ukiunguza mataili ambayo yalitupwa koromgoni na wananchi pia aliwataka wananchi kuchukua tahadhari kubwa majanga ya moto yanapotokea.

Komba alisema,walitumia muda mrefu kuuzima moto huo kwasababu ulikuwa mkubwa na iliwalazimu kutumia maji nyenye dawa (form compaund) kwaajili ya kuuzima moto huo.

Alisema,watu wanatabia ya kutupa vitu mbalimbali kwenye dampu kama chupa zenye gesi hivyo huwa ni rahisi sana kujitokeza kwa milipuko wakati moto unapowaka ndio maana huwa tunawaambia watu kukaa mbali na janga la moto linapotokea.

Aidha komba aliwataka wananchi kutoa taarifa kwa kikosi cha zima moto kunapokuwepo na janga la moto ili kuokoa mali za wananchi pia aliongeza kuwa ushirikiano wanaoupata kutoka kwea waandishi wa habari na wananchi umewafanya wao kufanya kazi kwa haraka.

0 comments: