Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Sunday, March 15, 2015

ZILE TETESI ZA sugu kutomjali mtoto jibu hili hapa__PICHA YAKE AKIWA NA MWANAE...X WAKE ASEMA WANAPIGA PICHA MARA KIBAO TU

Picha aliyoweka Faiza Ally Instagram ya Mhe. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ akiwa katika pozi na mwanaye Sasha.
MSANII wa filamu Faiza Ally ambaye amezaa na Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, leo amewatolea uvuvi watu waliokuwa wakijiuliza maswali kuhusu mwanaye Sasha na na baba yake.
Baada ya kuweka picha ya Sugu na mwanaye, Faiza Ally aliandika haya.
Kupita akaunti yake ya Instagram, Faiza ameweka picha na Mhe. Sugu akiwa na mwanaye Sasha na kuandika kuwa     "Mara nyingi huwa nawapiga picha mimi mwenyewe sema tu sipendi sana kurusha kwangu"
Na kwa wale waliokuwa wanauliza maswali juu yao, Faiza amewajibu hivi: "Ni kweli kuna wakati tulikuwa hatuelewani kabisa na wala hatukuwa tunaonana lakini kwa sasa tofauti zetu zimeisha hatuna ugomvi japo hatuko pamoja"

Faiza akiwa na Mhe. Sugu enzi hizo.
"Lakini mwisho wa siku huyo ndiyo baba Sasha na mzazi siku zote atakuwa mzazi tu, haijalishi tuna tofauti kiasi gani" Alimalizia kuandika msanii huyo asiyeishiwa vituko.
Baada ya kuwek picha hiyo wengi wa mashabiki wa Faiza walimpongeza kwa hatua hiyo huku wengine wakiwataka warudiane ili walee mtoto pamoja.

0 comments: