Asilimia 50 ya watu wazima nchini Japan hawashiriki katika tendo la ngono kulingana na utafiti, swala linalosababisha kupungua kwa idadi ya watu nchini humo.
Kati ya asilimia 48.3 waliohojiwa walisema kuwa hawakushiriki katika ngono kwa mwezi moja huku asilimia 50.1 ya wanawake wakijizuia kushiriki ngono.Takwimu zote zilipanda kwa asilimia 5 kutoka kwa ufatiti uliofanywa awali mwaka 2012.
Kati ya wanawake asilimia 23.8 walisema kuwa tendo la ngono linasumbua na asilimia 17.8 wakidai walikuwa wamechoka.
Swala jengine la kushangaza ni kuongezeka kwa idadi ya vijana ambao hawana hamu na tendo la ngono.Zaidi ya asilimia 20 ya wanaume walio kati ya umri wa miaka 25 na 29 hakuwa na hamu ya kufanya ngono.
0 comments:
Post a Comment