Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Wednesday, October 15, 2014

CHAMA CHA WALEMAVU WASIOONA WILAYANIN KILOLO, IRINGA WAMEISIHI JAMII KUWATAMBUA KATIKA KULETA MAENDELEO





Chama cha watu  wasioona mkoa wa Iringa waliopo  katika  wilaya ya  kilolo wamewasihi wananchi pamoja na wadau mbalimbali kuwaonesha ushirikiano katika shughuli za kimaendeleo.

Akizungumuza na blog hii leo mwenyekiti wa chama cha wasioona wilayani kilolo BI.Rusi Kisumbe alisema kuwa  mara nyingi  wamekuwa hawathaminiwi katika jamii na kuonekana  kama ni watu ambao hawawaezi kufanya kitu chochote katika hususani katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Mwenyekiti wa chama cha wasioona Wilaya ya Kilolo Mkoa wa Iringa Bi.Rusi Kisumbe  akiwa na mjumbe wa chama hicho Bw.Haruna Makete.

Aidha Bi. Kisumbe alisema, wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile kukosa ofisi za kuendeshea shughuli zao za kila siku, ubovu wa mazingira wanayoishi, ikiwa ni pamoja na kutopewa mikopo ambayo itawasaidi kujiendesha wenyewe kama chama.

Kwa upande wake mwanachama na mjumbe mtendaji wa chama hicho cha wasioona wilayani kilolo Bw. Haruna  Maketa nae  alielezea changamoto kubwa ambayo wao  wanayokutana nayo ni kutokupewa fursa za kutosha katika umiliki wa ardhi tatizo jambo linawakwamisha hasa kwenye suala la kilimo.

Hata hivyo Bi. Kisumbe aliwataka wadau kuwasaidia chama cha wasioona katika  wilaya ya  kilolo kwa kuwasaidia kwenye chama hicho ili kiweze kuendesha shughuli za kimaendeleo na kuwataka wanajamii kutowachukulia wao kama ni ombaomba kwa kuwa wao ni walemavu.


 

0 comments: