Ripoti nyengine ya maafisa hao iliotolewa na Gazeti la Washington Post pia ilitoa maoni kama hayo.
Lakini upande wa Bw Trump umepuuzilia mbali matokeo ya ripoti hiyo, ukisema hawa ni watu wale wale waliosema kuwa Sadaam Hussein anamiliki silaha za kuangamiza.
Maafisa wa Urusi kwa mra nyengine wamekana kuhusika na udukuzi wowote wa kumsaidia Trump katika uchaguzi huo.
Siku ya Alhamisi rais Obama alitaka uchunguzi kufanywa kufuatia misururu ya udukuzi wa mitandao inayodaiwa kutekelezwa na Urusi wakati wa uchaguzi.
Udukuzi huo ulilenga barua pepe za chama cha Democratic na mshauri wa mgombea wa urais Hillary Clinton.
SOURCE:BBC Swahili
0 comments:
Post a Comment