Muziki,Habari motomoto,MICHEZO,Maajabu,Picha Picha na mambo mengine mengi hapa ndani ya KALI ZA DJ YEYO

nongona

tangazo eligod

tangazo eligod

About the Author

CHECK me!!!!

CHECK me!!!!

Friday, August 21, 2015

MAAJABU:Ama kweli Ng'ombe hazeeki maini ONA Ndoa za wazee zatikisa Morogoro


SHANGWE! Katika tukio linalotokea kwa nadra, wazee kumi ambao wameishi kinyumba kwa miaka mingi,Jumamosi iliyopita walibariki ndoa zao katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Monica, lililopo Tungi mkoani Morogoro, huku zoezi hilo likitikisa kila kona ya mjini hapa.
Kwa mujibu wa padri aliyefungisha ndoa hizo, Ferdinand Mushi, tukio hilo lilifanyika baada ya ushawishi wa muda mrefu wa viongozi wa Kigango cha Mt. Clara kwa wazee hao, ambao awali walifanya doria ya nyumba hadi nyumba ili kubaini watu wanaoishi bila ndoa za Kikristo.http://api.ning.com/files/bGawF3RRkad2JxFbu7rVp9s5wSdnjcBLx-eD*N430c9GbcJWuKN1jb2r8UJYQDF-sG6gc3fztQXxDgxWjM3NvvfxeLhyp7i4/MoroNdoa.gif
“Naomba Vigango vingine hapa Morogoro na Tanzania kwa ujumla kuiga mfano wa Mt. Clara, ambao waliamua kuwapa semina na kukubali kufunga ndoa,” alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kigango hicho, Gilbert Robert alisema wao kama viongozi, wajibu wao ni kuwaelekeza waumini kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, kwani kabla ya kufanikisha zoezi hilo, walifanya sensa na kugundua uwepo wa familia 44 zinazoishi bila ndoa, lakini ni kumi tu kati yao ndiyo walikubali kubariki.
“Baadhi waligoma wakidai hawana fedha za kufanya sherehe, hivyo sisi Kigango tumeamua kuwafanyia sherehe kwenye ukumbi huu wa masista,” alisema mwenyekiti huyo.
Wakati wa sherehe hizo ukumbini, wanandoa hao, wapambe, ndugu na jamaa waliburudika kwa chakula aina ya pilau na soda, huku kukiwa na vituko vya hapa na pale ikiwa ni pamoja na mabusu ya kizee kutawala.
Baada ya sherehe hiyo, wakati wa kurejea makwao tulishuhudia baadhi yao wakitembea kwa miguu huku akina mama wakizikunja shera zao, ingawa pia baadhi yao waliondoka kwa bodaboda, tena wakiwa wamepakizana kwa staili maarufu ya mishikaki.

0 comments: